ETI MZEE MAGALI HAKUMBUKI IDADI YA FILAMU ALIZOCHEZA

KATIKA
hali iliyoonesha kushangaza wengi, hivi karibuni staa wa sinema za
Kibongo, Charles Magali ‘Mzee Magali’ alisema eti hakumbuki idadi ya
filamu alizoigiza wala majina yake.

Mzee
Magali aliibua kituko hicho wakati akibadili nguo kuingia kurekodi
filamu mpya ya Pasuko la Moyo ya Quick Promotions ambayo itaingia
barabarani Septemba 17, mwaka huu.
“Mimi kazi yangu ni kukamua tu, sijui nimeshacheza filamu ngapi,
sikumbuki hata majina yake, wanajua wenye filamu, ninayoijua ni hii ya
Pasuko la Moyo kwa sababu ni mpya, kwa hiyo kuanzia sasa naanza
kuzishika kichwani,” alisema mzee huyo kwa sauti kali
No comments:
Post a Comment