look around you

look around you
mysef

Saturday, August 31, 2013

MAHUSIANO

MAKOSA 10 WANAWAKE HUYAFANYA WAKIWA FARAGHA

Kitanda kina kanuni zake. Kuna makosa mengi hufanywa na wanawake, vilevile yapo ambayo wanaume huyafanya. Si sawa kuyaacha yaendelee kuwepo kwa sababu faragha ni hatua muhimu katika ukamilishaji wa kitu kinachoitwa penzi.
Uhusiano wa kimapenzi una wigo mpana. Kuna mambo mengi ambayo yakifanywa huufanya mwili uwe na afya. Hata hivyo, suala la faragha halipaswi kusahaulika, kwa maana ni chachandu madhubuti.
Tendo la faragha lina nguvu sana katika kuuweka hai uhusiano. Wapo watu ambao picha zilikuwa haziendi katika maisha ya kawaida lakini kila wakikutana kitandani, kila mmoja alimvulia kofia mwenzake.
Hii ina maana kuwa inawezekana mwenzi wako akawa dhaifu katika maeneo mengine lakini ‘maujuzi’ yake faragha, yakakufanya uwe mtulivu kwake.
Vivyo hivyo, nawe hakikisha unampatia mwezi wako katika eneo fulani ili hata akikufanyia visa, basi uwe na ukurasa wako ambao akiufikia ni lazima akuvulie kofia. Faragha ni uwanja huru ambao ambao hudhaniwa ni mgumu lakini ni rahisi sana.
Haihitaji msuli mkubwa wala nguvu kama za samba. Usidanganyike kwenda kutumia madawa ya kuongeza nguvu wala kwenda kwa waganga eti ndiyo wakuboreshee mvuto wako. Tuliza kichwa, soma kitendo chenyewe halafu hakikisha hufanyi makosa.
Katika makosa mengi ambayo wanawake huyafanya wakiwa faragha, ndani ya mada hii, nimeyaunganisha na kuyafanya yasomeke 10. Nikuhakikishie kuwa ukiyaepuka na kufuata mwongozo sahihi, utakuwa bora sana.
Mambo mengi hayahitaji taaluma, ni suala la kuushirikisha ubongo ili uamue kinachotakiwa. Mathalan; kuzungumza na mwenzi wako kumuuliza nini umfanyie ili afurahie tendo au kumwelewesha cha kufanya aweze kukupatia, haihitaji maarifa mengi au uwezo wa juu kiakili.
Kujifanya unajua sana husababisha wengi kuchemka. Achana na tabia ya kuhisi wewe umekamilika na kujidanganya kwamba unafahamu kila kinachotakiwa katika uwanja mahsusi wa faragha. Inakugharimu kiasi gani kuzungumza naye ili akujuze mahali hisia zake zilipolalia?
Yupo mwanamke ambaye tangu anazaliwa mpaka anakua, amekariri kwamba ukiwa faragha dawa ni kuzungusha ‘bakuli’ mwanzo mwisho. Matokeo yake, anakutana na mwenzi wake, badala ya kusoma mahitaji yake, yeye akili, nguvu na ujuzi wake wote anauelekeza katika nyonga tu. Mauno mtindo mmoja.
Hajui kwamba pengine mwenzi wake hapendi purukushani za kupanda na kushuka. Inapotokea wewe ni mtaalamu wa kucheza juu ya msumari (wana wa unyago mnaelewa), dakika 90 hushushi mzigo chini, ukidhani unamfurahisha, kumbe unageuka kero kwa mwezio.
Inaweza kutokea umekariri kuwa ukiwa katika utekelezaji wa sanaa ya faragha lazima uporomoshe mayowe. Japo ni nzuri katika kupata mrejesho (feedback) wa tendo lenyewe lakini si ajabu mwenzako hafurahii hilo. Zungumza naye tafadhali.
Hekima za tendo zinakataa ububu, lazima muwe mnaambiana mara kwa mara. Kama siku hajakutendea haki, mweleze waziwazi kwamba hajakufikisha. Ukimwacha afanye anachotaka na anachojisikia yeye, mwishowe haitakuwa na msisimko kwako.
Tengeneza utofauti wa makutano ya mbuzi na binadamu. Maana beberu huwa hajui maana ya kumwandaa jike. Anapojisikia kupanda anafanya hivyo na anapotosheka anashuka. Wewe na mwenzi wako hamna budi kuwa na nidhamu. Hisia ziheshimiwe.
Ikiwa mtatenda kwa makubaliano, kila mmoja akifuata maelekezo ya mwenzi wake, akitilia mkazo yale maeneo ambayo yametajwa katika mazungumzo kwamba ndiyo huleta raha, basi raha huwa raha kweli. Zingatia mambo 10 yafuatayo;Tuungane katika sehemu ya pili

MZEE MAGALI HAKUMBUKI KACHEZA MUVY NGAPI?

ETI MZEE MAGALI HAKUMBUKI IDADI YA FILAMU ALIZOCHEZA

KATIKA hali iliyoonesha kushangaza wengi, hivi karibuni staa wa sinema za Kibongo, Charles Magali ‘Mzee Magali’ alisema eti hakumbuki idadi ya filamu alizoigiza wala majina yake.
Mzee Magali aliibua kituko hicho wakati akibadili nguo kuingia kurekodi filamu mpya ya Pasuko la Moyo ya Quick Promotions ambayo itaingia barabarani Septemba 17, mwaka huu.
“Mimi kazi yangu ni kukamua tu, sijui nimeshacheza filamu ngapi, sikumbuki hata majina yake, wanajua wenye filamu, ninayoijua ni hii ya Pasuko la Moyo kwa sababu ni mpya, kwa hiyo kuanzia sasa naanza kuzishika kichwani,” alisema mzee huyo kwa sauti kali

RAY C IS COMING BACKKKKKK..........

copyrighted from global publishers

RAY C AHAHA KUONDOA MINYAMA UZEMBE, ABATIZWA KWA MAJI MENGI.

Hakika sexy lady kwenye Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ amepona na sasa anahaha kukata minyama uzembe baada ya kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya ‘unga’.
Ray C au Kiuno Bila Mfupa, juzikati alitupia picha kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram zikimuonesha akiwa ‘bize gym’ akifanya mazoezi makali kupunguza unene akijiandaa kurejea rasmi kwenye gemu.
Picha hizo zinamuonesha akikimbia kwenye mashine maalum ya kukimbilia, akifanya mazoezi ya viungo na nyingine akifanya mazoezi ya kukata tumbo ambapo mashabiki wake kwa asilimia kubwa walimpongeza kwa hatua hiyo.
“Kiuno Bila Mfupa umetishaaa…sasa umerudi enzi zile…bora ulivyoamua kufanya mazoezi,” yalisomeka sehemu ya maoni hayo.
Baada ya kupona na kuacha madawa ya kulevya kwa msaada wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete baada ya kutolewa kwenye magazeti ya Global akiwa hoi, sasa anasubiriwa kwa shauku na mashabiki wake wanaotamani kumuona stejini kwa mara nyingine.
Wakati gazeti hili linakwenda mitamboni lilipokea ‘nyiuzi’ kuwa Septemba 29, mwaka huu (Alhamisi) iliyopita, Ray C alibatizwa kwa maji mengi katika Kanisa la Sloam lililopo Bunju, Dar.tunakusubiri sana dada tumemiss sauti yako.

DIAMOND AND LINAH MHHHHHHHHHH.

Copyrighted from global

DIAMOND, LINAH TABIA MBAYA


Tabia mbaya! Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amenaswa na msanii mwenzake, Esterlina Sanga ‘Linah’ wakiwa kwenye mapozi ya kimahaba ambayo yametafsiriwa vibaya.
Katika tukio hilo lililojiri juzikati kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora ndani ya Tamasha la Serengeti Fiesta, Diamond alishuhudiwa akiwa amempakata Linah ndani ya basi huku mikono ya jamaa huyo ikishika maeneo nyeti.
Mara baada ya kutimba uwanjani hapo wakitokea hotelini tayari kwa kufanya shoo, Diamond na Linah walibaki kwenye basi wakiwa wamepakatana na hata msichana huyo alipomaliza shoo yake kali mishale ya saa 3: 00 usiku, alirejea mikononi mwa Diamond ambaye alimpachika mapajani.
Shushushu  aliwapiga chabo ‘wakifanya yao’ hadi Diamond alipokwenda stejini na kuangusha bonge la shoo huku akimwacha Linah mpweke.
Kwa mujibu wa mashuhuda, kama kweli mchumba wa Diamond, Penniel Mungwilwa ‘Penny’ anakubali mambo kama hayo, basi atakuwa na roho ngumu au moyo wa chuma.
alipohojiwa Linah kuhusu ishu hiyo, alifunguka: “Weweee…hakuna ni mapozi tu na wala usiandike hiyo habari.”
Siyo mara ya kwanza Diamond na Linah kuripotiwa wakiwa wamepozi kimahaba kwani mwaka jana walifanya hivyo wakiwa jijini Mbeya hivyo kutafsiriwa kuwa inaonekana ni katabia kao kabaya wanakaendekeza.

FASHION TONIGHT

Copywrighted from miss popular,
THE ALLY REHMTULLAH NIGHT HOPE NO ONE WANTS TO MISS IT,

You thought the Fashion Avenue is just a name?! Well,think again!!
 Ally Rehmtullah brings the Dar es Salaam famous street as a Fashion Avenue...quite LIVE!

 An outdoor event that gives the guests a taste of fashion in a classy environment and elegant settings
 Need I say more?

 The preps have been done...the models sharpened....the venue on point!
Looking forward to seeing you,tonight!!

urembo hot lulu in red lipssssssss


HotLulu
pendeza sanaaxoxo.

NI GK TENAAAAAAAAAAAA.

KAKA YETU GK ARUDI TENA GOOD TO BE BACK BROTHER

Baada ya ukimya wa miaka 6 "Baraka au Laana" yamrudisha tena GK


 Baada ya ukimya wa miaka sita bila ngoma wala interview, leo King Crazy GK akiwa amesindikizwa na East Coast Team nzima kuanzaia AY, Mwana FA, Buf G (Gizinga), Paulin Zongo, Yuzo pamoja na Snea, ameibuka na kudondosha single mpya "Baraka au Laana"  aliyomshirikisha Yuzo."Baraka au laana ni swali ambalo nimewaachai watanzania wajiulize, ni baraka au ni laana uzaliwa Afrika, unajua kitaka kujua kile anachokiwaza mwingine muulize swali, akianza kufunguka ndio utajua anawaza nini juu ya ulichomuuliza, so hili ni swali kwa Watanzania. tumekuwa tukiskia watu wakisema bora kuzaliwa paka Ulaya kuliko kuzaliwa binaadam Afrika, kwasababu kule wanyama wanatimiziwa haki zao kuliko sisi huku, sasa tujiulize is it true..amesema GK."

Hapa GK alikuwa anamzuka balaaa, alikuwa anachana verse yake kwenye wimbo wa "Hii Leo" walioufanya ECT, mara tu baada ya kufika  studio. AY, FA wote walichana verse zao.Hatari Sanaaaa
walikuja full full, studio ilikuwa kama party vile, full ma sparkling wine na ma champagne, ktoka kushoto ni Fetty, B12, Zero, FA, AY, Buff G (mwenye mask ya blue), Snare, GK, anaefata simjui na yule mrefuuuuuu ni Adam Mchomvu  
 

VIMBWANGA VYA MASTAA


Sean Kingstone ashitakiwa kwa kumbaka mtungo msichana mwenye miaka 20, ambaye alikuwa amelewa

Sean Kingston na walinzi wake (Bodyguard) wamemla mtungo msichana (20) aliekuwa amelewa, katika chumba cha Hoteli, 2010.

Carissa Capeloto  ambae kwa sasa ana miaka 22,  anadai  kulazimishwa kufanya ngono na Sean, walinzi wake na member wa bendi ya Sean katika hoteli iliyoko Seattle, Julai, 2010, baada ya yeye kuvuta bangi na kufuta shots 7-10 za vodka.
Capeloto - ambaye amewashitaki watu wote 3, anadai alialikwa katika chumba cha hoteli hiyo na Kingston kwa kukutana-na-kusalimiana (meet and greet) kufuatia tamasha la Bieber, ambapo Kingston pia alikuwa aki- perform, lakini wakati alipofika chumbani, Kingstone alikuwa ameshatupa kule kila kilichokuwa mwilini mwake (naked) yuko juu ya kitanda akimsubiri
Capeloto amedai kuwa mlinzi alimnyanyua na kumuweka juu ya Kingston, na wote watatu waliendelea  kumbaka wakati yeye alikuwa "ni wazi amelewa, na kutokuwa na uwezo wa kutoa ridhaa."
Capeloto anasema rafiki yake baadaye aliingia katika chumba na kumuokoa. Polisi waliitwa na Capeloto alipelekwa hospitali ambapo anasema yeye alikuwa akitibiwa kwa majeraha ya kimwili sambamba na ubakwaji.
Anasema maisha yake yameharibiwa, halali vizuri usiku, ana mood swings na anadai fidia ya dola mil 5 kima cha chini.
Kingstone amepeleka documents za kisheria zinazodai kuwa ngono waliofanya ilikuwa ni makubaliano kwa asilimia 100.
Kesi inatarajiwa kusikilizwa mwezi wa 9.

STORY YA PUNDA

JIFUNZE

Mpendwa,
Siku moja punda wa mkulima alianguka ndani ya kisima. Mnyama huyo alipiga kelele kinyonge kwa masaa kadhaa wakati mkulima akijaribu kufikiri nini cha kufanya.
 
Hatimaye, aliamua kwakuwa punda wake alikuwa mzee, na pia kisima hicho kilihitaji kufunikwa juu, Akaona hapakuwa na haja ya kumtoa.
 
Akaita majirani zake wote waje kumsaidia. Wao wote wakachukua makoleo na kuanza kuchota taka kwa koleo na kuzitupia ndani ya kisima.
 
Mara ya kwanza, punda aligundua nini kilikuwa kinatokea akapiga kelele kwa nguvu. Basi, ikawashanganza wale watu punda aliponyamaza ghafla!
Baada ya kutupa taka kadhaa kwenye hicho kisima. Huyo mkulima alishangazwa na kile alichokiona. Kwamba kila koleo la taka lililorushwa juu ya mgongo wa punda, punda alikuwa akifanya kitu cha kushangaza. Alikuwa akijitikisa ili taka zimwagike chini huku akipiga hatua moja kuja juu.

Kadri mkulima na majirani walivyoendelea kutupa uchafu kwa koleo juu ya punda yule, alizidi kutikisa mgongo wake na kupiga hatua moja kuja juu. Muda mfupi baadae, kila mtu alishangaa jinsi punda alivyozidi kutokeza ndani ya kisima na kuja juu.



FUNZO:
Maisha yatakutupia kila aina ya uchafu. Ili utoke nje ya kisima wahitaji kujitikisa na kuchukua hatua moja juu. Kila tatizo ulilonalo, ni jiwe la kukuwezesha kukanyaga na kupiga hatua kuja juu. Tunaweza kutoka nje ya kisima kirefu kwa kuongeza bidii ya kupiga hatua moja kuja juu bila kuacha na kutokata tamaa kamwe. Tikisa itikisa uchafu mbali na kuchukua hatua kuja juu.
Kumbuka kanuni 5 rahisi ili uwe na furaha:
1. Weka huru moyo wako mbali na chuki - Samehe.

2. Weka huru akili yako mbali na wasiwasi - Wengi hushindwa kabisa kipengele hiki.

3.Tosheka / rizika na ulichonacho.

4. Toa zaidi.

5. Tarajia vichache kutoka kwa watu lakini zaidi kutoka kwako mwenyewe.

Una uchaguzi wa aina mbili ...
i) Tabasamu na funga ujumbe huu,
ii) au tuma ujumbe huu kwa mtu mwingine ili ashiriki somo hili

Imetumwa na: Dr. Emeria A. Mugonzibwa - Mwanga.

LULU HUYOOOOOO,,,,,,,,


          

LULU AZINDUA  MOVIE MPYA - FOOLISH AGE





PROIN PROMOTIONS LTD
Imewaletea  movie mpya ya Lulu "Foolish Age"
Hii ni pamoja na kuzindua kampuni yao ya usambazaji wa movie za kibongo,
movie hiyo ambayo siku si nyingi itaingia mitaani yes lulu bado tunakukubali 
and still tutakusupport 



        

YA EID YALIKUWA MEMA

NAMSHUKRU MUNGU KWAKUNIWEZESHA EID HII NILIPATA NAFASI YA KUILA NA WATOTO YATIMA KATIKA KITUO FULANI NILIPATA FARAJA SANA JAMANI SINA MENGI YA KUSEMA HIVI PUNDE NTAZIMWAGA PICHA HIZO WAPENZI WANGU SUBIRINI